Kristo atarudi akiwa na kusudi gani?
Kabla Yesu Kristo hajapaa mbinguni mwaka wa
33 W.K., aliahidi kwamba angerudi. Alijilinganisha na mtu mashuhuri
aliyesafiri kwenda nchi ya mbali kisha akarudi na mamlaka ya kutawala
akiwa mfalme. Yesu atarudi ili kuwaletea wanadamu serikali bora.—Soma Luka 19:11, 12.
Yesu atawaletea wanadamu serikali bora
Kristo atarudi akiwa na mwili wa aina gani? Yesu alifufuliwa akiwa kiumbe wa roho asiyeonekana. (1 Petro 3:18) Kisha, akaenda mbinguni na kuketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu. (Zaburi 110:1)
Baadaye, Yesu aliletwa mbele ya Yehova Mungu, “Mzee wa Siku,” ambaye
alimpa mamlaka ya kuwatawala wanadamu. Yesu hatarudi kama mwanadamu,
bali kama Mfalme asiyeonekana.—Soma Danieli 7:13, 14.
Yesu atafanya nini atakapowasili?
Yesu atakapofika bila kuonekana pamoja na malaika
wake, atawahukumu wanadamu. Atawaangamiza watu waovu na kuwapa uzima wa
milele wale wanaomkubali kuwa Mfalme.—Soma Mathayo 25:31-33, 46.
Yesu atakapotawala akiwa Mfalme, ataigeuza dunia
iwe paradiso. Atawafufua wafu ili wafurahie kuishi katika Paradiso hiyo
itakayokuwa duniani.—Soma Luka 23:42, 43.


No comments:
Post a Comment