Friday, 20 December 2013

‘Fanyeni Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’


1, 2. Huenda mitume walikuwa wakifikiria nini kuhusu safari ya kwenda Yerusalemu?
‘MWEZI mchanga unaonekana waziwazi kwa sababu hakuna mawingu. Bila shaka, walinzi wa Yerusalemu waliuona mwezi huo jana jioni. Baada tu ya Sanhedrini kujua hilo, inatangaza kuanza kwa mwezi mpya wa Nisani. Kisha, watu wanapata habari hizo kupitia wajumbe au mioto inayowashwa kotekote kama ishara. Ni wazi kwamba Yesu anajitayarisha kwenda Yerusalemu ili afike kabla ya Pasaka.’

Siku Hii Itakuwa Ukumbusho Kwenu


Majibu ya Maswali ya Biblia



 Kristo atarudi akiwa na kusudi gani?

Kabla Yesu Kristo hajapaa mbinguni mwaka wa 33 W.K., aliahidi kwamba angerudi. Alijilinganisha na mtu mashuhuri aliyesafiri kwenda nchi ya mbali kisha akarudi na mamlaka ya kutawala akiwa mfalme. Yesu atarudi ili kuwaletea wanadamu serikali bora.—Soma Luka 19:11, 12.

Yesu Kristo—Tumkumbuke kwa Njia Gani?


Mwezi wa Desemba watu wengi ulimwenguni pote huona picha za Yesu akiwa mtoto. Akiwa amelazwa kwenye hori, yaani, sanduku kubwa linalotumiwa kulishia wanyama. Lakini je, tunapaswa kumkumbuka Yesu akiwa mtoto tu? * Acheni tuzungumzie njia muhimu zaidi ya kumkumbuka. Tunaweza kujifunza kutokana na jambo lililowapata wachungaji waliokuwa malishoni karibu na Bethlehemu usiku mmoja.

Thursday, 19 December 2013

Yesu Alizaliwa Lini?



Jibu la Biblia

Biblia haitaji tarehe hususa ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo, kama vitabu hivi vya marejezo vinavyoonyesha:
  • Tarehe halisi ya kuzaliwa kwa Kristo haijulikani.”— New Catholic Encyclopedia.
  • Tarehe hususa ambayo Kristo alizaliwa haijulikani.”— Encyclopedia of Early Christianity.
Ingawa Biblia haijibu moja kwa moja swali hili, ‘Yesu alizaliwa lini?’ inaeleza matukio mawili yanayohusiana na kuzaliwa kwake ambayo yanawafanya watu wengi wafikie mkataa wa kwamba hakuzaliwa Desemba 25.

Wednesday, 18 December 2013

BIBLIA INASEMA NINI KUHUSU KRISMASI?



Jibu la Biblia

Biblia haitaji tarehe ambayo Yesu alizaliwa, wala haisemi kwamba tusherehekee siku yake ya kuzaliwa. Kama vile kitabu McClintock and Strong’s Cyclopedia kinavyosema: “Mwadhimisho wa Krismasi haukuagizwa na Mungu, wala hautokani na AG [Agano Jipya].
Kinyume cha hilo, historia ya Krismasi inafunua kwamba inatokana na sherehe za kipagani. Biblia inaonyesha kwamba tunamchukiza Mungu ikiwa tunamwabudu katika njia ambayo yeye hakubali.—Kutoka 32:5-7.