‘MWEZI mchanga unaonekana waziwazi kwa sababu
hakuna mawingu. Bila shaka, walinzi wa Yerusalemu waliuona mwezi huo
jana jioni. Baada tu ya Sanhedrini kujua hilo, inatangaza kuanza kwa
mwezi mpya wa Nisani. Kisha, watu wanapata habari hizo kupitia wajumbe
au mioto inayowashwa kotekote kama ishara. Ni wazi kwamba Yesu
anajitayarisha kwenda Yerusalemu ili afike kabla ya Pasaka.’
Friday, 20 December 2013
Majibu ya Maswali ya Biblia
Kristo atarudi akiwa na kusudi gani?
Kabla Yesu Kristo hajapaa mbinguni mwaka wa
33 W.K., aliahidi kwamba angerudi. Alijilinganisha na mtu mashuhuri
aliyesafiri kwenda nchi ya mbali kisha akarudi na mamlaka ya kutawala
akiwa mfalme. Yesu atarudi ili kuwaletea wanadamu serikali bora.—Soma Luka 19:11, 12.
Yesu Kristo—Tumkumbuke kwa Njia Gani?
Mwezi wa Desemba watu wengi ulimwenguni pote huona
picha za Yesu akiwa mtoto. Akiwa amelazwa kwenye hori, yaani, sanduku
kubwa linalotumiwa kulishia wanyama. Lakini je, tunapaswa kumkumbuka Yesu akiwa mtoto tu?— *
Acheni tuzungumzie njia muhimu zaidi ya kumkumbuka. Tunaweza kujifunza
kutokana na jambo lililowapata wachungaji waliokuwa malishoni karibu na
Bethlehemu usiku mmoja.
Thursday, 19 December 2013
Yesu Alizaliwa Lini?
Jibu la Biblia
Biblia haitaji tarehe hususa ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo, kama vitabu hivi vya marejezo vinavyoonyesha:
- “
Tarehe halisi ya kuzaliwa kwa Kristo haijulikani.
”— New Catholic Encyclopedia. - “
Tarehe hususa ambayo Kristo alizaliwa haijulikani.
”— Encyclopedia of Early Christianity.
Ingawa Biblia haijibu moja kwa moja swali
hili, ‘Yesu alizaliwa lini?’ inaeleza matukio mawili yanayohusiana na
kuzaliwa kwake ambayo yanawafanya watu wengi wafikie mkataa wa kwamba
hakuzaliwa Desemba 25.
Wednesday, 18 December 2013
BIBLIA INASEMA NINI KUHUSU KRISMASI?
Jibu la Biblia
Biblia haitaji tarehe ambayo Yesu alizaliwa, wala
haisemi kwamba tusherehekee siku yake ya kuzaliwa. Kama vile kitabu
McClintock and Strong’s Cyclopedia kinavyosema: “
Mwadhimisho wa Krismasi haukuagizwa na Mungu, wala hautokani na AG [Agano Jipya].”
Kinyume cha hilo, historia ya Krismasi inafunua
kwamba inatokana na sherehe za kipagani. Biblia inaonyesha kwamba
tunamchukiza Mungu ikiwa tunamwabudu katika njia ambayo yeye hakubali.—Kutoka 32:5-7.
Subscribe to:
Comments (Atom)



